MAN CITY YAMSAJILI BONGE LA BEKI TOKA ATHLETIC BILBAO

Aymeric Laporte is all smiles as he signs his first contract as a Manchester City player
Vinara wa Ligi kuu nchini England Manchester City wamevunja rekodi ya Usajili wao kwa kumsajili beki wa kimataifa wa Ufaransa Aymeric Laporte kutoka Athletic Bilbao Kwa ada ya uhamisho paundi milioni 57.

Laporte mwenye miaka 23 anakuwa mchezaji wa Kwanza wa Manchester City kusajiliwa kwa kiasi kikubwa cha fedha na amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu akivunja rekodi iliyowekwa na Kevin De Bryune aliyesajiliwa kwa paundi milioni 55.

Laporte anayecheza nafasi ya beki wa kati anasajiliwa na kocha Pep Guadiola baada ya mawindo ya muda mrefu kutaka kumsajili mpaka ijumaa ambapo walifikia makubaliano ya kumsajili na leo Jumanne kutia saini mkataba wa kuichezea Manchester City.

HAWA NDIYO WACHEZAJI WALIOSAINIWA KWA PESA NYINGI MAN CITY.

Aymeric Laporte - Â£57m 
Kevin De Bruyne - Â£55m
Benjamin Mendy - Â£52m 
John Stones - Â£50m 
Kyle Walker - Â£50m 
Raheem Sterling - Â£49m 






No comments

Powered by Blogger.