TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA


DAVID DE GEA

Wakala wa kipa wa Man United David De Gea Jorge Mendes amekataa kupinga uwezekano wa kipa huyo kuhamia Real Madrid na kusema kila kitu kinawezekana.
(Marca )

GABRIEL PAULISTA

Manchester United wanajiandaa kukuuteka usajili wa Arsenal kwa kumsajili beki wa Villareal Gabriel Paulista mwenye miaka 24 ambaye Arsenal wametangaza kuanza mazungumzo naye kutaka kumsajili.
(Daily Star)

DOUGLAS COSTA

Chelsea wako katika mkakati wa kumsajili kiungo wa  Shakhtar Donetsk mwenye miaka 24 Douglas Costa.
(Sun)

DARREN FLETCHER

Bosi wa West Brom Tony Pulis amethibitisha kuwa anataka kuwasajili winga wa Wigan Callum McManaman na kiungo wa Manchester United  Darren Fletcher, 30.
(Times )

PATO

QPR wamepewa mshambuliaji wa Zamani wa AC Milan ambaye anaichezea  Corinthians Alexandre Pato, 25.
(Daily Mail)

RAHEEM STERLING


Kocha wa Liverpool  Brendan Rodgers anategemea winga wake Raheem Sterling mwenye miaka 20, atasaini mkataba mpya na klabu hiyo hivi karibuni.
. (Sky Sports)

AARON LENNON

Hull City wanamwania winga wa Totenham Aaron Lennon mwenye miaka 27 ambaye anajipanga kuondoka White Hart Lane mwezi huu.
(Hull Daily Mail)

KEVIN DE BRYUNE:

Kiungo wa zamani wa Chelsea anayekipiga katika klabu ya Wolfsburg Kevin de Bruyne mwenye miaka  23, ambaye amehusishwa na kutakiwa na Arsenal na Manchester United amesema hana mpango wa kurudi katika ligi kuu ya England.
 (Daily Star)

 CHICHARITO


Matumaini ya Mashambuliaji wa Man United Javier Hernandez (Chicharito) kusajili moja kwa moja na Real Madrid mara mkataba wake wa mkopo utakapoisha yameanza kufifia baada ya Real Madrid kuonyesha kutokua na uhitaji katika nafasi ya mshambuliaji na hii itamlazimu mshambuliaji huyo kurudi Old Trafford mwishoni mwa msimu.
(Daily Express)

No comments

Powered by Blogger.