LIVERPOOL YAKAMILISHA USAJILI WA RICKIE LAMERT WA SOUTHAMPTON


Rickie Lambert akiwa na Uzi wa Southampton


Mshambuliaji wa England Rickie Lambert ( Pichani) anajiandaa kupata vipimo vya afya katika kukamilisha ndoto yake ya kujiunga na Liverpool akitokea Southampton kwa ada ya uhamisho Paundi milioni 4.

Lambert mwenye umri wa miaka 32 alishawahi kuichezea Liverpool miaka mitano akiwa mchezaji Chipukizi kipindi ameanza kucheza soka, amezichezea pia Bristol Rovers,Stockport na Rochdale.
Msimu ulioisha katika ligi kuu Nchini England lambert amekua mhimili mkubwa wa kikosi cha Southampton baada ya kufunga magoli 14 akitoa pasi za mwisho 10 katika mechi 39 akitengeneza kombinesheni nzuri kati yake Adam Lallana na Jay Rodrigous.

Kama Kila kitu kikienda sawa basi Lambert atasafiri kuelekea Merseyside baada ya mechi ya leo Ijumaa ya kirafiki kati ya  England dhidi ya Peru kupimwa afya na kutambulishwa Rasmi kama mchezaji wa Liverpool.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

2 comments:

  1. Hii Southampton itapukutishwa yote kwa wachezaji wao wote kusajiliwa na timu kubwa

    ReplyDelete
  2. Kweli kabisa hawa south ya mtoni wanabomolewa bila huruma.

    ReplyDelete

Powered by Blogger.