HAPATOSHI TAIFA LEO HUKU SAMATA HUKU ALI KIBA

Nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samata sambamba na mwanamuzi wa Muziki wa kizazi Kipya Ali Kiba Leo jioni katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wataviongoza vikosi yao katika mechi ya hisani kuchangia madawati mkoa wa Dar es Salaam.

Samata na Kiba wamefikia hatua hiyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika uboreshaji wa elimu jijini Dar es Salaam.

Wawili hao wamechagua vikosi vyao ambavyo wataviongoza Leo kuanzia saa 10 jioni kucheza mechi hiyo inayotadhamiwa kuleta burudani kubwa kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam huku Mgeni rasmi akiwa ni Waziri wa habari Sanaa na Michezo Mheshimiwa Harrison Mwakyembe.

No comments

Powered by Blogger.