SOUTHGATE AMTEUA HARRY KANE NAHODHA MPYA UINGEREZA
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgate amemtangaza Mshambuliaji wa
Tottenham Harry Kane kuwa nahodha
mpya wa kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza
kitakacho shiriki michuano ya kombe la dunia itakayo anza mwezi ujao
nchini Urusi.
Southgate ametangaza maamuzi hayo leo kupitia vyombo vya habari huku zikiwa
zimebaki siku 22 kuanza kwa michuano hiyo mikubwa duniani kwa ngazi ya mataifa
" Harry ni kiongozi mzuri ndani na nje ya timu
na ana sifa zote za kuwa kiongozi ," alisema Soughagate.
Wiki iliyopita mchezaji wa zamani wa Chelsea na timu
ya taifa ya uingereza Frank Lampard alimpigia chapuo Harry Kane kuwa nahodha wa
timu ya taifa ya Uingereza
No comments