MANAHODHA WA NCHI PINZANI WAUNGANA KUMUOMBEA MWENZAO AFUNGULIWE NA FIFA

Kuelekea fainali za
kombe la dunia zinazotarajiwa kuanza kurindima mwezi ujao, nahodha watatu
kutoka kundi c linalojumuisha nchi za Ufaransa, Peru, Denmark na Australia
wameungana na kuiandikia FIFA barua yenye lengo la kuomba FIFA wamruhusu
nahodha Paolo Guerrero wa Peru acheze kombe la dunia.
Guerrero amekumbwa na kifungo cha kutojihusisha na soka cha miezi 14 baada ya vipimo kuonesha anatumia dawa za kulevya aina ya cocaine.
Dawa hizo zinasemekana ziliwekwa kwenye chai aliyokunywa Guerrero na manahodha hao wanadai kuwa Guerrero alikunywa chai hiyo bila kuja kama imewekewa cocaine
Katika barua hiyo
wanaeleza "tunaamini kuwa hukumu ikilegezwa kwa muda itakuwa ni jawabu
tosha kwa Paolo na Peru"
Hukumu hiyo kwa Paolo
imeamsha hisia tofauti katika mitaa mbalimbali nchini Peru, wananchi
wamekusanyika katika maeneo mbalimbali wakijaribu kuishinikiza FIFA imruhusu
Nahodha Wao na Mfungaji Wao aweze kucheza fainali hizo.
Raisi wa taifa la Peru ameiingilia kati na kuiagiza serikali kumsaidia Paolo Guerrero ili kuhakisha anacheza kombe la Dunia mwezi ujao
Hebu angalia kipande
hiki hapa chini huu ukiwa ni mkusanyiko wa wananchi wa peru katika uwanja wa
mpira wa Estadio Nacional.
Tribuna norte casi lleno en la marcha pacífica por Paolo Guerrero pic.twitter.com/hFDRiHmf0L— Silvana Palacios (@SilvanaVanita94) May 20, 2018
No comments