HUYU HAPA MRITHI WA WENGER PALE ARSENAL

Aliekuwa kocha wa Paris St Germain Unai Emery anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha mpya wa Arsenal baada ya washika bunduki hao wa London kubadili uamuzi wa kumkabidhi nahodha wao wa zamani Mikel Arteta kiti hicho kilichoachwa na Arsene Wenger


Arteta mwenye umri wa miaka 36 alionekana kuwa tayari kutwaa mikoba hiyo baada ya mazungumzo na viongozi wa klabu ya Arsenal huku akiwa ni chaguo la CEO Ivan Gazidis lakini inaonekana kama maamuzi yamebadilika mwishoni.

Emery  mwenye umri wa miaka 46 aliachana na PSG ya Ufaransa mwishoni mwa msimu wa 2017/18 akiwa ameshinda kombe moja la la Ligue 1, vikombe viwili vya Coupes de France, viwili vya Coupe de la Ligue pamoja na viwili vya Supercup katika misimu miwili aliyodumu hapo.

Emery alisafiri hadi London jana Jumatatu kwa ajili ya mazungumzo lakini www.wapendasoka.com inatambua kuwa alifanya mazungumzo pia na West Ham lakini iwapo mambo yatamwendea vema na Arsenal basi atasaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo.


No comments

Powered by Blogger.