SOKA LA VIJANA MKOANI IRINGA LAPIGWA JEKI
Kampuni
za Alishati Investment na Puma Energy wamejitokeza kudhamini kituo cha kukuzia
vijana cha mkoani Iringa (Iringa Football Academy).
Alishati atakuwa mfadhili wakati Puma ni
mdhamini ambaye atatoa vifaa kwa ajili ya mechi na mazoezi pamoja na kugharamia
mafuta ya usafiri kwa mechi za ugenini.
Udhamini huo utakiwezesha kituo hicho kufanya
kazi kwa weredi na kuzalisha wachezaji wazuri ndani ya mkoa wa Iringa.
Mkurugenzi Mtendaji wa IFA, Ally Msigwa
amemtangaza Kocha Mshindo Msola kuwa Mkurugenzi wa ufundi wa kituo hicho.
Mkurugenzi huyo pia ametangaza wajumbe saba wa
bodi ya IFA akiwemo Waziri wa mambo ya nje Dk. Augustino Mahiga.
No comments