LUKAKU HATIHATI KUIKOSA BRIGHTON
Mshambuliaji
wa Manchester United, Romelu Lukaku anaweza akakosa mchezo wa ligi kuu ugenini
dhidi ya Brighton siku ya Ijumaa.
Kinara huyo wa mabao ya United alipata maumivu
ya enka katika mchezo dhidi ya Arsenal wikiendi iliyopita uliomalizika kwa
ushindi wa 2-1 Old Trafford.
Raia huyo wa Ubelgiji alifanyiwa vipimo jana
Jumatatu na sasa anasubiri majibu ili kuona kama ameumia kwa kiasi gani.
Meneja wa United, Jose Mourinho amesema kama
Lukaku atakuwa hajaumia sana atarejea uwanjani mapema.
"Sijui ameumia kwa kiasi gani, sidhani kama
atakuwa nje ya uwanjani kwa muda mrefu, anapenda kucheza muda wote.
“Lukaku hachoki, na kama jeraha litakuwa
ni dogo hajali anarudi mazoezini, nilimfanyia mabadiliko sababu alishindwa
kucheza," alisema Mourinho.
No comments