YANGA KUSAFIRI KESHO KUWAFATA WAARABU


Mabingwa wa ligi kuu na wawakilisha pekee waliosalia katika michuano ya kimataifa Yanga wanatarajia kuondoka nchini kesho Mei 3 kuelekea nchini Algeria kwa ajili mchezo wa kwanza wa makundi wa kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger.
Msemaji wa klabu ya Yanga, Dismas Ten amesema wameamua kuondoka siku tatu kabla ya mchezo ili wachezaji kuzoea mazingira na mwisho wa siku wapate ushindi.
Yanga itaondoka Alhamisi kuelekea Algeria ikipitia Dubai kwa ajili ya mchezo wao  wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya USM Alger siku ya jumapili tarehe 6
Yanga iko kundi D ikiwa na Gor Mahia ya Kenya, Rayon Sports ya Rwanda, pamoja na USM Alger

No comments

Powered by Blogger.