YANGA YAWAANGAMIZA WAHABESHI KOMBE LA SHIRIKISHO
wakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa Yanga wameibuka na ushindi wa bao 2-0 katika mechi yao ya kwanza hatua ya mwisho ya mtoano dhidi ya Walita Dicha ya Ethiopia.
Yanga walianza mchezo wa Leo vizuri baada ya kupata bao la mapema zaidi sekunde ya 30 tu baada ya mpira kuanza likifungwa na kiungo wake Raphael Daudi bao lililodumu mpaka mapumziko.
Kipindi cha pili kiliwapa nguvu na ari zaidi Yanga kuongeza wigo wa ushindi na kufanikiwa kupata bao la Pili dakika ya 54 likifungwa na kichwa na Emmanuel Martin
Matokeo hayo ni faida kubwa Kwa Yanga kwani wanahitaji sare tu katika mchezo wao wa marudiano siku 10 zijazo mjini Adis Ababa Ethiopia.
Kama Yanga watafanikiwa kushinda mechi zote mbili na kuwatoa Wahabeshi hao basi watatinga hatua ya makundi katika michuano hiyo ya pili kwa ukubwa katika ngazi ya klabu barani Afrika.
Yanga walianza mchezo wa Leo vizuri baada ya kupata bao la mapema zaidi sekunde ya 30 tu baada ya mpira kuanza likifungwa na kiungo wake Raphael Daudi bao lililodumu mpaka mapumziko.
Kipindi cha pili kiliwapa nguvu na ari zaidi Yanga kuongeza wigo wa ushindi na kufanikiwa kupata bao la Pili dakika ya 54 likifungwa na kichwa na Emmanuel Martin
Matokeo hayo ni faida kubwa Kwa Yanga kwani wanahitaji sare tu katika mchezo wao wa marudiano siku 10 zijazo mjini Adis Ababa Ethiopia.
Kama Yanga watafanikiwa kushinda mechi zote mbili na kuwatoa Wahabeshi hao basi watatinga hatua ya makundi katika michuano hiyo ya pili kwa ukubwa katika ngazi ya klabu barani Afrika.
No comments