PAWASA AIPA NAFASI SIMBA KUIFUNGA YANGA JUMAPILI


Mlinzi wa zamani wa timu ya Simba, Boniface Pawasa amekiri mechi ya watani wa jadi ni ngumu na haitabiliki  lakini anaamini Wekundu hao wanaweza kuibuka na ushindi mbele ya Yanga Jumapili.

Mlinzi huyo amesema Simba wapo kwenye kiwango bora kwa sasa na wana wachezaji wenye uwezo wa kubadili matokeo muda wowote lakini amesisitiza lolote linaweza kutokea.

Pawasa ameongeza kuwa mechi ya watani inaweza ikakuweka katika nafasi nzuri kwenye medani ya soka lakini pia inaweza kukupoteza kabisa katika ramani kwahiyo wachezaji wanapaswa kutambua hilo.

"Mechi ya Simba na Yanga asili yake huwa haitabiliki ni ngumu sana, safari hii Simba ipo vizuri zaidi ya Yanga kama wachezaji wake watacheza kwa kujituma naamini wataibuka na ushindi.

"Simba ina safu imara ya ushambuliaji ambayo ndio imefunga mabao mengi mpaka sasa na wanajua kutengeneza nafasi ingawa haimaanishi haiwezi kupoteza mchezo," alisema Pawasa.

Miamba hiyo itakutana Jumapili katika uwanja wa Taifa mtanange unaotarajiwa kuanza saa 10 jioni.

No comments

Powered by Blogger.