ARSENAL YABANWA NYUMBANI, MARSEILLE KICHEKO EUROPA LEAGUE
Arsenal
imeanza Kwa sare ya bao 1-1 katika mchezo wake wa kwanza wa hatua ya nusu
fainali ya michuano ya kombe la Europa maarufu kama Europa League dhidi ya
Atletico Madrid katika uwanja wa Emirates jijini London.
Dakika
zote za kipindi cha kwanza hazikuzaa matunda licha ya Atletico Madrid kuwa
pungufu kuanzia dakika ya 10 baada ya mchezaji Sime Vrsaljko kutolewa nje Kwa
kadi Nyekundu kufuatia madhambi aliyoyafanya dhidi ya Alexandre Lacazette ikiwa
ni kadi ya pili ya njano.
Kipindi
cha Pili kila timu ilijitahidi kufunguka kupata bao na walikua ni Arsenal
waliotangulia kupata bao dakika ya 61 likifungwa na Alexander Lacazette Kwa
kichwa akiunganisha mpira wa krosi ya Jack Wilshere.
Antoine
Griezman aliwanyanyua mashabiki wa Atletico Madrid akifunga bao safi na muhimu
katika hatua ya kusaka nafasi ya kutinga fainali dakika ya 82 baada ya makosa
ya safu ya ulinzi ya Arsenal ikiongozwa na Laurent Koscienly.
No comments