ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE: ARSENAL NA ATLETICO MADRID ZAKWEPANA

Arsenal were drawn against Russian side CSKA Moscow in Friday's Europa League draw 

Arsenal na Atletico Madrid zimepangwa katika mechi tofauti kwenye droo ya hatua ya Robo fainali ya michuano ya Kombe la Europa league ambayo ni ya pili kwa ukubwa katika hatua ya klabu barani Ulaya.
 Arsenal na Atletico Madrid ni kati ya timu ambazo mara nyingi zilikua zikionekana katika ligi ya mabingwa lakini msimu huu imekua tofauti baada ya Atletico kushika nafasi ya tatu kwenye kundi lake hivyo kushindwa kuendelea na ligi ya mabingwa wakati Arsenal wao waliingia huku kupia ubingwa wa kombe la FA walioupata msimu uliopita.

Baada ya kuitoa AC Milan sasa Arsenal itacheza dhidi ya CSKA Moscow, Atletico Madrid yenyewe ikipangwa kucheza dhidi ya Sporting lisbon ya Ureno, RB Leipzig ikipangwa kucheza dhidi ya Olympique Marseille wakati Lazio kutoka Italia ikipangwa kucheza dhidi ya FC Salzburg ya Austria.

Mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa Alhamisi ya April 6 na marudiano ni baada ya wiki moja yani April 12 mwaka huu 2018.

No comments

Powered by Blogger.