KUIONA SIMBA "YA KIMATAIFA" JUMAPILI NI BUKU 5 TU


Vinara wa ligi kuu Soka Tanzania bara Wekundu wa Msimbazi Simba Jumapili ya wiki hii wanaerejea katika anga za kimataifa watakapoikaribisha Gendarmerie Nationale ya Djibouti katika mchezo wa hatua ya kwanza ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Majira ya Saa 10 jioni huku Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ally Hassan Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi

Viingilio katika mchezo huo vitakuwa VIP A Tsh 30,000 wakati VIP B itakua ni TSh 20,000,  Jukwaa la rangi ya chungwa (Orange) utakua ni 10,000 na mzunguko ambao viti vyake ni vya kijani kiingilio itakuwa buku tano tu (Tsh 5,000)

Akiongea na waandishi wa Habari Msemaji wa klabu hiyo, Hajji Manara amewataka wapenzi na mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi kuishangili timu yao ili kuwapa nguvu na hamasa wachezaji kuibuka na ushindi.

No comments

Powered by Blogger.