BUKU 5 TU KUWAONA YANGA NA ST LOUIS


Yanga sc imetaja viingilio vitatu katika mchezo wake wa hatua ya awali wa klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Saint Louis FC ya Shelisheli siku ya Jumamosi katika Uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Kiingilio cha chini katika mchezo huo kwa majukwaa ya mzunguko itakuwa 5000 wakati VIP B na C Itakuwa Sh 7000 huku VIP A ikiwa Sh 10000

Waamuzi wa mchezo huo wanatarajiwa kutoka Ethiopia na Kamishna wa mchezo akitokea nchini Namibia, Mwamuzi wa kati atakuwa Belay Tadesse Asserese akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Tigle Gizaw Belachew na mwamuzi msaidizi namba mbili Kinfe Yilma Kinfe wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Amanuel Heleselass Worku na Kamishna Frans Vatileni Mbidi.

No comments

Powered by Blogger.