HAWA HAPA WANAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA AFRICA KWA MWAKA 2017

Shirikisho la soka barani Afrika limetoa orodha ya wachezaji 30 watakaowania taji la mchezaji bora wa soka barani Afrika kwa mwaka 2017.
Mshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta anaechezea Krc Genk ya Nchini Ubeligiji nae ameorodheshwa kwa mara ya pili
Mshindi wa mwaka 2016 Riyad Mahrez wa Algeria hakuorodheshwa katika orodha hiyo.
Kati ya wachezaji 30 waliorodheshwa ni saba pekee ambao hawachezi soka yao barani Ulaya, huku kipa wa Misri Essam EL Hadary akiorodheshwa.
Washindi wa mataji hayo watatangazwa katika mji mkuu wa Ghana Accra mnamo tarehe 4 mwezi January 2018.
Kura zitakazopigwa na makocha, wakurugenzi wa kiufundi kutoka mataafa mbali mbali pamoja na wanachama wa kiufundi wa Caf na kamati endelebu mbali na jopo la waandishi zitabaini washindi.

 Orodha kamili ya wanaowania tuzo hiyo

Vincent Aboubakar (Cameroon & Porto), Karim El Ahmadi (Morocco na Feyenoord), Christian Atsu (Ghana & Newcastle), Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon na Borussia Dortmund), Eric Bailly (Cote d'Ivoire na Manchester United), Cedric Bakambu (DR Congo na Villareal), Keita Balde (Senegal & Monaco), Christian Bassogog (Cameroon na Henan Jianye), Yves Bissouma (Mali na Lille), Khalid Boutaib (Morocco na Yeni Malatyaspor), Yacine Brahimi (Algeria na Porto), Essam El Hadary (Egypt na Al Taawoun), Junior Kabananga (DR Congo na Astana), Fackson Kapumbu (Zambia na Zesco), Naby Keita (Guinea na RB Leipzig), Ali Maaloul (Tunisia na Al Ahly), Sadio Mane (Senegal na Liverpool), Moussa Marega (Mali na Porto), Victor Moses (Nigeria na Chelsea), Youssef Msakni (Tunisia na Al Duhail), Michael Olunga (Kenya na Girona), Fabrice Ondoa (Cameroon na Sevilla), Denis Onyango (Uganda na Mamelodi Sundowns), Thomas Partey (Ghana na Atletico Madrid), Mohamed Salah (Egypt na Liverpool), Mbwana Samata (Tanzania na Genk), Jean Michel Seri (Cote d'Ivoire na Nice), Percy Tau (South Africa na Mamelodi Sundowns), Bertrand Traore (Burkina Faso na Lyon), William Troost-Ekong (Nigeria na Bursaspor)

No comments

Powered by Blogger.