ERASTO AWAFUNIKA OKWI, NIYONZIMA SIMBA, MWEZI OKTOBA

Mchezaji kiraka wa timu ya Simba Erasto Nyoni atapokea kitita cha sh laki tano (500,000) baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba wa mabingwa hao wa kombe la FA.

Erasto ambaye mara kadhaa kocha Joseph Omog amekuwa akimtumia kama beki wa kulia au kushoto yupo kwenye kiwango bora msimu huu ambapo mchango wake ni mkubwa kikosini.

Licha ya uwepo wa nyota wenye majina makubwa kama Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, John Bocco na Shiza Kichuya lakini jina la Nyoni huwezi kukosa kulisikia kila baada ya kumalizika kwa mchezo wa Wekundu hao.

Erasto ni mmoja wa wachezaji wa Simba wanaotarajiwa kuwepo kwenye kikosi kitachocheza na Mbeya City mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya mwishoni mwa juma.


Nyoni ndiye mchezaji aliyedumu muda mrefu kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' ambapo huu ni mwaka wa 10 bado anaendelea kujumuishwa.

No comments

Powered by Blogger.