TSHISIMBI WA YANGA AWASILI NA KWENDA MOJA KWA MOJA KAMBINI PEMBA


Kiungo mpya wa Yanga, Rasta raia wa Congo, Papii Kabamba Tshishimbi tayari amewasili mjini Pemba kwa ajili ya kujiunga na wenzake ambao wanajiandaa na mchezo wa ngao ya jamii dhidi ya Simba utakaopigwa katika uwanja wa taifa Agosti 23.

Kiungo huyo kutoka Mbabane Swallows ya Swaziland alisaini mkataba wa miaka miwili na yanga hivi karibuni lakini inaelezwa kwamba alikua na tatizo katika passport yake ambalo lilikua likishughulikiwa.

Kuwasili kwa kiungo huyo mkabaji kunashusha presha za mashabiki wa Yanga ambao walikua wakimsubiri kwa hamu nyota huyo, hasa wakati huu ambao wanajiandaa kuwakabili watani zao wa jadi.

No comments

Powered by Blogger.