JAMES MSUVA AFUZU MAJARIBIO MBAO FC.
James
Msuva ambaye ni mdogo wake na nyota wa Yanga na Taifa Stars Saimon Msuva,
ameibukia katika mazoezi ya Mbao FC ya Mwanza ambako amefanya majaribio na
kufuzu.
James ambaye kwa nyakati tofauti amewahi
kuvichezea vikosi vya vijana vya Simba na Yanga aliichezea JKT katika msimu
uliopita wa ligi kuu.
Kocha wa Mbao Etienne Ndayiragije amesema
amewajaribu wachezaji wengi kwa ajili ya kujenga kikosi chake ambacho kimeondokewa
na nyota kadhaa.
Ndayiragije amesema wapo waliofuzu majaribio
hayo akiwemo James hivyo kinachofuata ni viongozi kusaini naye mkataba ili
akitumikie kikosi hicho msimu ujao.

No comments