SHIRIKISHO LA SOKA BARANI AFRIKA CAF LIMEPATA MDHAMINI MPYA

Shirikisho la soka barani Afrika CalAF limepata mdhamini mpya wa mashindano yake baada ya kumalizika kwa mkataba na kampuni ya mawasiliano ya Orange.



Orange walikua wakiidhamini michuano yote inayoandaliwa na CAF tangu mwaka 2009 mpaka mwaka huu ambao nao waliwapokea MTN

CAF Imeingia ubia na kampuni ya mafuta ya TOTAL yenye makao makuu yake nchini Ufaransa inayofanya biashara zake katika nchi mbalimbali Barani Afrika mkataba ambao thamani yake haijawekwa wazi.

TOTAL ITADHAMINI MASHINDANO YAFUATAYO
  • Kombe la mataifa ya Afrika
  • Ligi ya Klabu Bingwa Afrika
  • Kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN)
  • Super Cup ya Afrika
  • Kombe la shirikisho barani Afrika
  • Kombe la la mataifa ya Afrika kwa Wanawake
  • Kombe la Futsal Afrika
  • Kombe la mataifa ya Afrika wachezaji wa chini ya miaka 23
  • Kombe la mataiafa ya Afrika wachezaji wa chini ya miaka 20
  • Kombe la mataifa ya Afrika wachezaji wa chini ya miaka 17

No comments

Powered by Blogger.