JULEN LOPETEGUI NDIYO KOCHA MPYA WA HISPANIA

Chama cha soka nchini Hispania imemtangaza kocha wa zamani wa Porto na timu ya vijana ya Hispania Julen Lopetegui kama kocha wao mkuu.



Julen mwenye miaka 49 anachukua nafasi ya Vicente del Bosque aliyeamua kuachia ngazi baada ya michuano ya Euro 2016.

Julen amewahi kuichezea Spain nafasi ya golikipa wakati akicheza soka alikua pia akipewa nafasi ya kwenda kuifundisha Wolverhampton ya England.

Amewahi pia kuifundisha timu ya taifa ya Spain chini ya miaka 19 miaka 20 na miaka 21 na amefanikiwa kushinda ubingwa wa Ulaya mwaka 2012 chini ya miaka 19 na badae ubingwa wa Ulaya chini ya miaka 21 akiwa na wachezaji kama David de Gea, Koke, Isco na Thiago Alcântara.

Alitimuliwa na katika kikosi cha FC Porto mwezi January baada ya matokeo mabaya na tangu wakati huo amekua hana timu.




No comments

Powered by Blogger.