SIMBA YAENDELEZA DOZI TAIFA,SAFARI HII YAIPIGA MGAMBO "MKONO"
Dozi zimeendelea kutolewa na Simba Sc katika mashindano mbalimbali ikiwa na kocha wake mpya Jackson Mayanja baada ya jioni hii kuifumua Mgambo JKT bao 5-1
Simba ambayo haijawahi kufungwa mchezo wowote chini ya kocha Mayanja imeonekana kuzidi Kuimarika baada ya kutoa kichapo hicho kwa Mgambo katika mfululizo wa mechi za ligi kuu Tanzania bara
Pambano hilo lililopigwa katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam na kuvuta hisia za mashabiki wengi ilishuhudia Hamis Kiiza akifunga bao la mapema kabisa baada ya kutumia udhaifu wa mabeki wa Mgambo na kufunga kabla ya Mwinyi Kazimoto na Ibrahim Ajib hawajafunga na mchezo huo kwenda mapumziko matokeo yakiwapa ushindi Simba wa bao 3-0.
Kipindi cha pili Simba walikianza taratibu huku wakimtumia sana Mkude na Majabvi kutibua mipango ya Mgambo na kufanikiwa kupata mabao mawili zaidi moja likifungwa na Danny Lyanga na Hamis Kiiza huku Mgambo nao walijitutumua na kufunga bao pekee kupitia kwa Fulyzulu Maganga
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 39 sawa na Azam fC lakini Azam wao wana faida ya mechi mbili mkononi baada ya mechi zao kusogezwa mbele huku Yanga ambao wamelazimishwa sare na Prisons http://wapendasoka.blogspot.com/2016/02/penati-yaiokoa-yanga-isipate-kipigo.html ikiongoza ligi ikiwa na pointi 40
Simba ambayo haijawahi kufungwa mchezo wowote chini ya kocha Mayanja imeonekana kuzidi Kuimarika baada ya kutoa kichapo hicho kwa Mgambo katika mfululizo wa mechi za ligi kuu Tanzania bara
Pambano hilo lililopigwa katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam na kuvuta hisia za mashabiki wengi ilishuhudia Hamis Kiiza akifunga bao la mapema kabisa baada ya kutumia udhaifu wa mabeki wa Mgambo na kufunga kabla ya Mwinyi Kazimoto na Ibrahim Ajib hawajafunga na mchezo huo kwenda mapumziko matokeo yakiwapa ushindi Simba wa bao 3-0.
Kipindi cha pili Simba walikianza taratibu huku wakimtumia sana Mkude na Majabvi kutibua mipango ya Mgambo na kufanikiwa kupata mabao mawili zaidi moja likifungwa na Danny Lyanga na Hamis Kiiza huku Mgambo nao walijitutumua na kufunga bao pekee kupitia kwa Fulyzulu Maganga
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 39 sawa na Azam fC lakini Azam wao wana faida ya mechi mbili mkononi baada ya mechi zao kusogezwa mbele huku Yanga ambao wamelazimishwa sare na Prisons http://wapendasoka.blogspot.com/2016/02/penati-yaiokoa-yanga-isipate-kipigo.html ikiongoza ligi ikiwa na pointi 40
No comments