WALICHOFANYIWA AFRICAN SPORTS NA SIMBA TAIFA HAWATAKAA WASAHAU
African Sports ya Tanga kwa mara ya kwanza Ikicheza katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam tangu kuanzishwa kwake ilijikuta ikipigwa bao 4-0.
Simba SC ambayo inaendeleza Wimbi lake la ushindi chini ya kocha Jackson Mayanja Ikicheza mechi ya tatu katika ligi na kupata ushindi huo mnono.
Hamis Kiiza alifunga mabao mawili, Hassan Kessy na Haji Ugando waliifunga Simba bao moja moja na kufanya mchezo huo kumalizika kwa ushindi wa bao 4-0 ambao Simba walipata.
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 36 katika nafasi ya tatu pointi 3 nyuma ya Yanga na Azam zinazoongoza ligi hiyo.
Hii ni mechi ya nne kwa kocha mpya wa Simba Jackson Mayanja katika mashindano yote kwanza aliamua na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa, Akawafunga Jkt Ruvu bao 2-0 Kisha Akawafunga Burkina Faso bao 3-0 katika kombe la Shirikisho na leo kushinda bao 4-0 dhidi ya African Sports.
Amefunga magoli 10 na hajafungwa goli lolote.
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 36 katika nafasi ya tatu pointi 3 nyuma ya Yanga na Azam zinazoongoza ligi hiyo.
Hii ni mechi ya nne kwa kocha mpya wa Simba Jackson Mayanja katika mashindano yote kwanza aliamua na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa, Akawafunga Jkt Ruvu bao 2-0 Kisha Akawafunga Burkina Faso bao 3-0 katika kombe la Shirikisho na leo kushinda bao 4-0 dhidi ya African Sports.
Amefunga magoli 10 na hajafungwa goli lolote.
No comments