LIGI KUU ENGLAND LEO : NAFASI YA TIMU ZA MANCHESTER KURUDI KILELENI

Raundi ya 16 ya ligi kuu nchini England inaanza leo kwa mechi 6 kupigwa katika viwanja 6 tofauti nchini England.

Ni nafasi nyingine tena kwa timu za jiji la Manchester Yani Manchester City ambao watakua nyumbani kuikaribisha Swansea na Manchester United ambao watakua ugenini kuwavaa AFC Bournemouth Kuongoza msimamo wa ligi hiyo kwa siku ya leo.


Timu zote hizo zina pointi 29 huku Manchester City wakiwa katika nafasi ya tatu na Manchester United wakikamata nafasi ya nne katika msimamo na kama timu zote zitashinda au mojawapo kushinda itafikisha pointi 32 sawa na vinara Leicester City ambao wao watacheza Jumatatu dhidi ya Chelsea.

Mechi ya mapema leo itazikutanisha Norwich City watakaokua nyumbani kuwaalika Everton huku mechi ya AFC Nournemouth na Man United ikiwa ndiyo mechi ya mwisho Jumamosi ya leo.

RATIBA KAMILI


  • 15:45. Norwich City vs Everton
  • 18:00. Crystal Palace vs Southampton
  • 18:00. Manchester City vs Swansea City
  • 18:00. Sunderland vs Watford 
  • 18:00. West Ham vs Stoke City 
  • 20:30. AFC Bournemouth vs Manchester United


NOTE: MUDA HUU NI KWA SAA ZA AFRIKA MASHARIKI

No comments

Powered by Blogger.