MIWANI PANA YA EDO ~ SABABU 5 ZA KUAMINI KWANINI YANGA ILIFUNGWA NA SIMBA KATIKA MECHI YA NANI MTANI JEMBE
Nani mtani Jembe? nadhani baada ya tambo na majigambo ya zaidi ya mwezi
mmoja sasa hatimaye imejulikana kuwa Simba ndiyo mtani jembe baada ya kushinda
mechi yake dhidi ya Yanga kwa jumla ya goli 3-1.
Viunga vingi vya jiji la Dar Es Salaam jana vilipambwa na bendera nyingi za
timu hizo hasa zaidi Yanga ambao walikua wakiongoza katika kukusanya pesa
katika shindano lililochezeshwa na Wadhamini bia ya Kilimanjaro kabla ya mchezo
uliopigwa Uwanja wa Taifa.
Jambo kubwa lililosababisha Yanga kufungwa ni kuzidiwa kimchezo japokua
miwani yangu pana iliweza kuangalia mambo mengine matano ambayo pengine
yalisababisha Yanga kupoteza mchezo huo
· Kujiamini kupita kiasi kwa wachezaji,mashabiki na hata viongozi.
Ligi kuu Tanzania bara imesimama kwasasa mpaka tarehe 25 huku Yanga
wakiongoza na Simba wako katika nafasi ya 4 na Yanga wakionekana kufanya vizuri
sana katika mzunguko wa kwanza huku Simba wakimaliza mzunguko wa kwanza kwa
kusuasua. Kisha Simba wakaingia katika mgogoro mkubwa uliopelekea kutimuliwa
kwa makocha wa timu hiyo. Siku chache kabla ya mechi ya Mtani Jembe Yanga
wakamsajili aliyekua mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi na kutangaza kama
atacheza katika mchezo huo.
Matukio yote hayo yanaweza kukuonyesha kwa jinsi gani Yanga walivyokua
wamejiamini hii iliwapa mwanya wa kubweteka kama wangeshinda goli nyingi tu
wakati Simba wao njia pekee kwao kupunguza migogoro ilikua ni kushinda hivyo
basi timu iliandaliwa mahususi kwa ushindi huku uzoefu wa kocha msaidizi
Selemani Matola ambaye amekaa amekaa muda mrefu na kikosi cha vijana wa Simba
ambao wengi wako kikosi cha wakubwa sasa kama Singano, Mkude n.k
· Umri wa Wachezaji
Ukiangalia kwa haraka kikosi cha Yanga kimesheheni wachezaji wengi ambao
umri wao ni mkubwa kiuhalisia tofauti na Simba ambao wametumia vijana wengi
ambao ndo kwanza wanaanza kuchipukia katika soka.
Hii inawapa faida Simba kwani Vijana hao wengi wanatafuta mafanikio lakini kwa Upande wa Yanga wachezaji wengi wameshafikia kikomo angalia mchezaji kama Juma Kaseja,Ngassa n.k hawa wameshawika sana nchi hii na hapo ndipo naamini kama umri wao pia umeshasogea.
Hii inawapa faida Simba kwani Vijana hao wengi wanatafuta mafanikio lakini kwa Upande wa Yanga wachezaji wengi wameshafikia kikomo angalia mchezaji kama Juma Kaseja,Ngassa n.k hawa wameshawika sana nchi hii na hapo ndipo naamini kama umri wao pia umeshasogea.
· Kuwa na wachezaji wengi waliokua wakicheza Simba
Hii sababu inaweza kuonekana ni ya kijinga ila ina maana sana ukiiangalia
kwa undani swala hili utagundua kama uwepo wa wachezaji wengi ambao
walishaichezea Simba unawafanya wachezaji hao kucheza kwa uoga hasa kwa
kukumbuka yaliyomtokea kipa wa Timu hiyo Barthez siku Yanga walipotoka sare ya
3-3 na Simba katika ligi.
Hapo ndipo utakubaliana nami baada ya makosa aliyoyafanya Juma Kaseja jana
na kupelekea Simba kushinda goli la 3 lakini kwa upande wa Simba wao hawana
kitu hicho wachezaji walijiamini na kufata vyema maelekezo ya kocha.
· Ushindi wa Goli 5 ambazo Simba iliwahi kuwafunga Yanga
Kila mara zinapotokea mechi za Simba na Yanga wazo kubwa wanaloingia nalo
Yanga uwanjani ni kulipiza kisasi cha magoli yale 5-0 ambayo Simba waliyapata
wakiifunga Yanga. Simba wao wazo lao kubwa ni kupata ushindi tu hata uwe wa bao
moja lakini Yanga wao wanataka ushindi tena mkubwa wa kuzidi zile 5-0 ili
kuwaridhisha mashabiki wao na viongozi pia. Miwani yangu imechunguza na
kutafakari kama hilo laweza kua ni mojawapo ya sababu iliyopelekea Yanga
kupoteza mchezo huo.
· Usajili usio na Tija
Kuna vitu vingine viongozi wa timu hizi kubwa wanapaswa kubadilika hasa
katika swala la usajili. Mara nyingi tumeona usajili umekua ukifanywa
kuwafurahisha mashabiki bila kupata maoni ya kocha wa timu.
Yanga imemsajili Emmanuel Okwi hivi karibuni wakati huo huo
walishamrudisha kundini Mrisho Ngasa hii inaifanya Yanga kufikisha
wachezaji wasiopungua 8 katika safu ya ushambuliaji hii inawapa faraja
mashabiki lakini kwa timu haina tija. Jambo lingine linaloambatana na hilo
ambalo mshikaji wangu Allen kaijage amelipinga ni kwamba wakati Usajili
ukifanyika wanaosajiliwa wanalipwa pesa nyingi sana ikiwaacha waliopo sio tu
wanalipwa kidogo lakini pia wanakosa namba hii kwa wachezaji Wabongo ambao
hawajafikia "level" za Proffesionalism wanaweza kucheza chini ya
kiwango ili kufikisha ujumbe kwa Uongozi.
Kwa haraka kabisa Miwani Pana ya Edo inaamini kua hizi ni kati ya sababu za
chache kati ya nyingi ambazo pengine zimepelekea Yanga kupoteza mchezo wa Nani
Mtani Jembe japokua makosa ya Uwanjani ndio yababu kubwa.
....... Imetayarishwa na Edo Daniel Chibo





No comments