YANGA VS AZAM NI VITA YA KUGOMBEA NAFASI YA PILI TAIFA LEO


Pazia la Ligi kuu Soka Tanzania bara msimu wa mwaka 2017/2018 linafungwa Leo Kwa timu zote 16 kucheza katika mechi 8 zitakazoamua mustakabali wa timu zote kwenye ligi hiyo kubwa kabisa katika ngazi ya vilabu hapa Tanzania.

Macho na masikio yatakua hasa katika mechi itakayoamua mshindi wa pili lakini pia timu itakayoungana na Njombe Mji kushuka daraja.

Azam FC Ikiwa na pointi 55 katika nafasi ya pili itakuwa Mgeni wa Mabingwa wa Kihistoria wa ligi hiyo Yanga wanaoshika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 52 Kwa hali ilivyo Azam FC wanahitaji sare tu kuweza kushika nafasi ya pili huku Yanga wao ambao siku za hivi karibuni wamekuwa wakisua sua watahitaji ushindi ili kuweza kumaliza katika nafasi ya pili.

Mechi ya awali baina ya timu hizo ilimalizika Kwa Yanga kushinda Kwa bao 1-0 katika uwanja wa Azam Complex Chamazi goli pekee la Gadiel Michael Mbaga.

Katika balaa la kushuka daraja Maji Maji ya Songea ambayo itacheza dhidi ya Mabingwa Simba kwenye uwanja wao wa nyumbani wanahitaji ushindi ili kusalia katika ligi hiyo wakiwa na pointi 23 point moja juu ya Njombe Mji na Ili Maji Maji isalie ligi kuu msimu huu inatakiwa kuifunga Simba Leo bao 5-0 Halafu waombee Ndanda yenye pointi 26 ipoteze mchezo wake dhidi ya Stand United pale Mtwara. 

No comments

Powered by Blogger.