AWADHI AKUBALI MZIKI WA NDANDA AKIRI WALISTAHILI KUFUNGWA


Nahodha wa timu ya Mwadui FC, Awadhi Juma amekiri kuwa katika mchezo wa jana dhidi ya Ndanda FC walizidiwa kila idara na walistahili kupoteza.

Mwadui ilikubali kipigo cha mabao 3-0 katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Nangwanda Sijaona na kurejesha matumaini ya kusalia kwenye ligi msimu ujao.

Kiungo huyo wa zamani wa Simba alisema wapinzani wao walicheza vizuri hasa kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata mabao yote matatu.

Awadhi aliongeza kuwa kipindi cha pili walijitahidi kutulia na kutuliza presha ya Ndanda lakini walishindwa kupata bao hata kufutia machozi.

"Ndanda walicheza vizuri na walistahili kushinda mechi ya jana, tutajipanga katika mechi ya mwisho ya kufungia msimu dhidi ya Njombe Mji," alisema Awadhi.

Katika mchezo wa jana mabao ya Ndanda yalifungwa na nahodha Jacob Massawe, Mrisho Ngassa na Tibar John.

No comments

Powered by Blogger.