VALDERDE ATAJA SABABU ZA KUWAACHA BENCHI MESSI, SUAREZ
Meneja wa Barcelona, Ernesto Valverde ametetea
maamuzi yake ya kufanya mabadiliko ya kikosi cha kwanza na kupelekea
kulazimishwa sare ya mabao 2-2 Celta Vigo jana usiku.
Mabao ya Ousmane Dembele na Paco Alcacer yalitosha
kuisawazishia Barca baada ya Jonny Otto na Iago Aspas kuifungia Celta Vigo huku
Sergi Roberto alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Nyota Lionel Messi na Luis Suarez walianzia benchi
katika mchezo huo wakati vinara hao wakicheza mechi 33 za La liga bila
kupoteza.
"Ni kweli tulifanya mabadiliko kadhaa katika
kikosi, kuna wachezaji ambao hawatumiki sana wamecheza na wameonyesha uwezo
mkubwa, hilo jambo zuri kwetu," alisema Valverde.
Barcelona itakutana na Sevilla katika mchezo wa
fainali wa Copa del Rey siku ya
Jumamosi.


No comments