UCL : BARCELONA YAENDELEA KUNUFAIKA NA MAGOLI YA KUJIFUNGA MSIMU HUU
Vinara wa ligi kuu Soka nchini Spain klabu ya Barcelona Jana usiku ilipata ushindi wa bao 4-1 katika mchezo wake wa hatua ya kwanza ya Robo fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya AS ROMA.
Ikiwa nyumbani Barcelona iliendelea kunufaika na magoli ya kujifunga baada ya kupata mabao mawili ya Kujifunga katika ushindi huo wa jana.
Daniele De Rossi na Konstantinos Manolas wa AS Roma walijifunga katika mechi hiyo kuwafanya Barcelona kufikisha goli 5 msimu huu ambazo wamezipata baada ya timu pinzani kujifunga ikiwa ndiyo timu pekee ambayo imepata faida hiyo msimu huu katika ligi ya mabingwa Ulaya.
Gerard Oique na Luis Suarez nao walifunga bao moja kila moja kwa upande wa Barcelona huku Edin Dzeko akiifungia AS Roma bao pekee katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Nou Camp.
Messi alikabidhiwa ngao maalumu ya kufikisha mabao 100 katika ligi ya mabingwa Ulaya |
No comments