HIZI NDIZO SABABU ALIZOTOA PEP GUADIOLA BAADA YA KICHAPO TOKA KWA LIVERPOOL

Liverpool 3-0 Man City: Salah, Oxlade and Mane score in first-half
Masaa machache baada ya Kukumbana na kichapo cha bao 3-0 kutoka kwa Liverpool, Kocha wa Manchester City Pep Guadiola ametoa sababu ambazo zilipelekea timu yake kupoteza mchezo huo muhimu wa kwanza katika hatua ya Robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya katika uwanja wa Anfield.


Aidha Pep hakuweka wazi sababu ya kupoteza mchezo huo kuwa ni uvamizi uliofanywa na mashabiki katika bus walilopanda kuelekea katika mchezo huo lakini anasema wachezaji wake walitoka kimchezo kutokana na tukio hilo akifananisha na tukio la msimu uliopita la wachezaji wa borussia Dortmund.

Mohammed Salah, Alex-Oxlade Chamberlain na Sadio mane walifunga mabao ya Liverpool jana ambayo yanaifanya kwenda katika mchezo ujao ikihitaji sare tu au kutofungwa zaidi ya bao 2-0 ili kufuzu hatua ya nusu fainali.

No comments

Powered by Blogger.