BEKI MWINGINE WA AZAM KUPELEKWA AFRIKA KUSINI


Mlinzi wa kati wa timu ya Azam FC, Yakub Mohammed anatarajiwa kupelekwa nchini Afrika Kusini kwa ajili ya uchunguzi wa mguu wake uliokuwa umevunjika.

Mwezi uliopita mlinzi mwingine Daniel Amoah alipelekwa nchini humo kupata matibabu ya goti ambapo mpaka sasa anaendelea kuuguza maumivu yake.

Yakub tayari ametolewa bendeji gumu (P.O.P) mguuni kwake lakini Daktari wao Mwanandi Mwankemwa amesema mchezaji huyo anahitaji uchunguzi kabla ya kuanza mazoezi mepesi.

Msemaji wa klabu hiyo, Jaffer Idd amesema mchezaji ataondoka nchini Mei mosi kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya uchunguzi wa jeraha lake.

"Yakub anatarajia kuondoka nchini Mei mosi kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya uchunguzi wa mguu wake kwa mujibu wa ushauri wa daktari wetu Mwanandi," alisema Jaffer.

Wakati huo huo kikosi cha Azam kimeomdoka leo  jijini Dar es Salaam kuelekea Morogoro kwa ajili ya mchezo wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar utakaochezwa siku ya Jumamosi.

No comments

Powered by Blogger.