KOCHA WA DR CONGO AWATAJA SAMATA, MSUVA NA ULIMWENGU


Kocha wa timu ya Taifa ya DR Congo, Ibenge Florent amesema haifahamu vizuri timu ya Tanzania lakini wachezaji watatu ndio anawajua ambao ni nahodha Mbwana Samata, Simon Msuva na Thomas Ulimwengu.

Kocha Ibenge amekiri kuwa mchezo wa kesho dhidi ya Taifa Stars utakuwa mgumu na anatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wenyeji.

Ibenge ameongeza kuwa moja ya sababu kuchagua kucheza na Stars ni kutokana na ukaribu pia Tanzania ina wachezaji wengi vijana wenye vipaji ambao watawapa ushindani.

"Sijui vizuri soka la Tanzania lakini nawajua Samata, Msuva na Ulimwengu lakini naamini kuna wengine wazuri," alisema Ibenge.

Mchezo huo ambao utapigwa kwenye uwanja wa Taifa utaanza saa 10 jioni.

No comments

Powered by Blogger.