COASTAL NA KMC ZAPANDA LIGI KUU


Timu KMC ya Dar es Salaam na wagosi wa kaya Coastal Union zote za kundi B zimeungana na JKT Ruvu kupanda ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2018/2019 baada ya kuibuka na ushindi katika mechi za mwisho zilizopigwa leo

KMC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jktt Mlale katika uwanja wa ugenini mkoani Songea
Bao pekee la Kmc limefungwa na Abdulhalim Humud katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo na kudumu mpaka dakika 90

Mechi Nyingi iliokuwa yakusisimu ilikuwa kati ya wagosi wa Tanga Coastal Union na Mawezi Market ya Morogoro mchezo uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Wagosi wakaya wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mawezi Market ya Morogoro na kufikisha pointi 26, mabao ya Coastal yalifungwa na Raizan Hafidh na Athuman Idd 'Chuji'

KMC NA Coastal wameungana maafande wa JKT Ruvua kupanda ligi kuu msimu ujao kutoka kundi A baada ya kufikisha pointi 34 wakiwa na mechi moja mkononi.
Matokeo kamili ya mechi za FDL zilizochezwa leo

Mbeya Kwanza 3-1 Polisi Dar
Mufindi United 1-2 Polisi Tanzania
JKT Mlale 0-1 KMC
Mawenzi Market 0-2 Coastal Union

No comments

Powered by Blogger.