SIMBA: NJOONI MUWEKEZE NYARAKA ZIKO TAYARI
Kamati inayoshughulikia masula ya zabuni ya klabu ya
Simba imetangaza kukamilika kwa nyaraka za mwaliko wa awali (Expression of
Interest) na kuwataka wanachama wenye sifa kujitokeza.
Mkutano mkuu maalum wa klabu hiyo uliofanyika Agosti
20 mwaka huu ulipitisha azimio la kuanzisha na kutekeleza mchakato wa uwekezaji
uliopitiswa.
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti huyo,
Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema nyaraka hizo zimekamilika na amewataka
wanachama wenye nia ya dhati ya kutaka kuwekeza kujitokeza kwa wingi.
Zoezi la kuchukua nyaraka hizo litakamilika Oktoba
18 ambalo litatangazwa kwenye vyombo vya habari ili kutoa fursa kwa wazabuni
watarajiwa kujiandaa, kukamilisha nyaraka muhimu na kufanya mashauriano kabla
ya kuwasilisha. Zoezi hilo litachukua siku 10.
Jaji Mihayo alisema "Nyaraka za mwaliko wa
zabuni zimekamilika. Niwakaribishe wanachama wa klabu ya Simba wenye sifa
kujitokeza kabla ya kufungwa kwa zoezi hili".
Mwenyekiti huyo pia alisema watakuwa wanatoa taarifa
kupitia vyombo vya habari katika kila hatua ya mchakato huo mpaka apatikane
mshindi.
No comments