WENGER AWEKA KANDO UBAHIRI, AMSAJILI LACAZETTE KWA PESA NDEFU

French striker Alexandre Lacazette has been confirmed as an Arsenal player 
Klabu ya Arsenal jana Ilikamisha uhamisho wa Mshambuliaji Alexandre Lacazette kwa Ada ya Uhamisho wa kihistoria katika klabu hiyo wa paundi milioni  53 akitokea Olimpic Lyon ya Ufaransa.


Msambuliaji huyo mwenye uwezo mkubwa wa kuzifumania nyavu alikua jijini London tangu Jumanne kwaajili ya vipimo vya afya kusaini mkataba na kukamilisha uhamisho huo.

Lacazette amesaini mkataba wa miaka miatano kuichezea Arsenal ambao ni mabingwa wa Kombe la FA.

Lacazette poses with his new manager, Arsene Wenger, after moving to Arsenal

Huu ni uhamisho wa kwanza mkubwa kwa klabu hiyo ukivunja rekodi ya Uhamisho wa mesuit Ozil wa paundi milion 42.5 mwaka 2013.

Lyon wamepata kiasi cha paundi milioni 46 taslimu huku paundi milioni 7 zitalipwa na Arsenal kutokana na maendeleo ya mchezaji.

lacazette mwenye miaka 26 ameifungia lyon mabao 136 katika mechi 289 na ujio wake pengine ukafanya mshambuliaji Olivier giroud aondoke klabuni hapo West ham na Everton wakimtolea macho.

No comments

Powered by Blogger.