LWANDAMINA AREJEA TAYARI KWA MAWINDO YA MSIMU MPYA.

Kocha wa Yanga George Landamina amewasili nchini jana kutokea Zambia alikokua kwa mapumziko baada ya msimu uliopita ambapo aliwaongoza Yanga kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Kuwasili kwa kocha huyo kumeondoa minong'ono iliyokuwepo miongoni mwa mashabiki wa soka nchini kwamba kocha huyo hatorejea kuwanoa mabingwa hao kwa msimu mwingine.

Baada ya kurejea, Lwandamina amesema atakaa na viongozi wa Yanga kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali kuhusu maandalizi ya timu hiyo kama yalivyopendekezwa katika ripoti yake ambayo tayari alishaiwasilisha kwao.

Yanga wamekua wakiendelea na usajili wa wachezaji sambamba na kuwasainisha mikataba mipya wale ambao mikataba imemalizika ambao kwa mujibu wa viongozi wa klabu hiyo ni kwamba wanasajili kwa mapendekezo ya kocha wao

No comments

Powered by Blogger.