YANGA WANYOOSHA MIKONO JUU, WATANGAZA KUMSHINDWA NIYONZIMA.
Mkataba wa Niyonzima na Yanga utamalizika mwishoni mwa mwezi huu na wapendasoka.com inafahamu kwamba mazungumzo yalikua yakiendelea kati yao huku Simba nao wakiwa wameweka donge nono mezani kwa ajili ya kumnasa nahodha huyo msaidizi wa Yanga.
Taarifa hiyo ni ishara kwamba sasa Niyonzima atavaa jezi za rangi nyekundu na nyeupe msimu ujao kwa dau linalotajwa kuwa ni zaidi ya shilingi milioni 100 za kitanzania.

No comments