OKWI KUTUA JUMAMOSI NA KUSAINI MIWILI SIMBA


Mchezaji nyota Emmanuel Okwi keshokutwa Jumamosi atatua nchini akitokea Uganda tayari kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba.

Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa Okwi kurejea Simba kutokana na kuitumikia timu hiyo kwa mapenzi mapenzi makubwa na mafanikio pia.

Usajili huo unakuja siku mbili baada ya taarifa kutoka kuwa Simba imekamilisha usajili wa kiungo fundi kutoka Yanga Haruna Niyonzima.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hanspope amewaambia Waandishi wa Habari kuwa mchezaji huyo atatua nchini Jumamosi na kusaini mkataba wa miaka miwili.

"Nilikuwa Uganda wiki iliyopita nikafanya mazungumzo na Okwi tukakubaliana kila kitu na  keshokutwa Jumamosi atatua nchini na kusaini mkataba wa miaka miwili."

No comments

Powered by Blogger.