LICHA YA KULIPIWA KILA KITU, TBS YAPIGA 'STOP' NYASI ZA UWANJA WA SIMBA NA HIZI NDIZO SABABU

Image result for NYASI ZA UWANJA WA SIMBA
Zile ndoto za mashabiki wa Simba kuweza kupata uwanja wao zimeendelea kuota mbawa baada ya kushindwa kupatikana kwa Nyasi bandia za klabu hiyo ambazo zilikua zimekwama muda mrefu bandarini kufuatia kucheleweshwa kulipiwa Ushuru kwa mamlaka ya mapato Tanzania TRA.

Tayari Simba walishalipa fedha zilizokuwa zikitakiwa na TRA pamoja na gaharama za utunzaji wa nyasi hizo lakini wakiwa wanajiandaa kwaajili ya kuzipeleka Bunju katika uwanja husika Shirika la Viwango Nchini Tanzania TBS liliibuka na kudai risiti halisi za nyasi hizo na Simba kushindwa kuzitoa kwani walikua na Vivuli tu vya risiti hizo na hata zilipofatiliwa Nchini China bado mpaka sasa imeshindikana kupatikana.

Taarifa ambazo www.wapendasoka.com Imezipata zinaeleza kwamba kwa kukosa huko kupata risiti halisi ya nyasi hizo Simba wanatakiwa kulipa faini ya milioni 37 Swala ambalo halijapatiwa ufumbuzi ndani ya klabu hiyo na huenda swala hilo likachukua muda mwingi zaidi mpaka TBS watakaporuhusu kuchukuliwa nyasi hizo.

Aidha hati ya Ukaguzi wa nyasi hizo ulishafanyika na Simba wana kivuli cha ukaguzi huo ambacho ndicho kilichopelekea kusafirishwa kwa nyasi hizo.

WITO WETU:

Kama Wapenda Soka Tungependa kuona swala hili linamalizika kwa maendeleo ya mpira wetu Tanzania ni vyema Viongozi wa Simba wakamshirikisha Waziri wa habari Sanaa utamaduni na Michezo ili kuweza kupata ufumbuzi wa jambo hili.

No comments

Powered by Blogger.