SIMBA YAISHITAKI TFF KWA FIFA

Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club  imeamua kuliburuza Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) hadi katika mahakama ya usuluhishi ya FIFA (CAS) kwa ajili ya kupata haki yake kufuatia suala la kupokwa pointi tatu kufuatia Kagera Sugar kumchezesha mchezaji mwenye kadi tatu za njano.
Rais wa klabu hiyo Evans Aveva alisema kuwa sababu tatu zilizotolewa na Kamati ya Katiba Sheria na Hadhi za Wachezaji hazikuwa na mashiko kwani suala la mchezaji kucheza akiwa na kadi tatu ni kosa kwa mujibu wa kanuni.

Rais Aveva amewaambia waandishi wa habari makao makuu ya klabu hiyo kuwa timu yake ya Simba imekuwa ikionewa na TFF kutokana na maamuzi mbalimbali yanayotolewa ndiyo maana wakaamua kupeleka malalamiko yao FIFA.

Simba ina subiri kupewa barua na (TFF) inayo onyesha kupokwa pointi hizo ili kuweza kupeleka malalamiko yao (CAS) kwa ajili ya kupata alama hizo ambazo wanasema ni halali kwao.

No comments

Powered by Blogger.