MAYANGA ATEUA MANAHODHA
Kocha Mkuu wa timu wa Taifa, Salum Mayanga amemteuwa
Himid Mao na Jonas Mkude kuwa manahodha wasaidizi huku akimuwenguo cheo hicho
John Bocco.
Akizungumza na.... Afisa Habari wa Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas alisema baada ya kufanya mabadiliko ya benchi
la ufundi, halitafanya mabadiliko kwa nahodha mkuu ambaye ataendelea kubaki na
Mbwana Samatta.
Alisema mabadiliko hayo yatafanyika kwa wasaidizi
hao baada ya kutoitwa na Bocco katika kikosi cha timu.
"Mabadiliko hayo yamefanyika kwa wasaidizi
pekee, hivyo Samatta ataendelea na majukumu yake katika mechi za Fifa ambapo
michuano ya CHAN yakisimamiwa na Himid pamoja ma Mkude," alisema Alfred.
Alisema Samatta anatarajia kuingia leo saa 4 usiku
na Farid Mussa akiingia saa 10 Alfajir na kesho kwenda kupimwa Afya zao ikiwemo
mapigo ya moyo kabla kuwavaa wapinzani wao Bostwana jumamosi uwanja wa Taifa.
No comments