WALIOPANGA MATOKEO LIGI DARAJA LA KWANZA HUKUMU YAO KESHO JUMAMOSI
Kamati inakutana kwa ajili ya kumalizia shauri la upangaji wa matokeo Ligi Daraja la Kwanza (StarTimes League) kundi C inayozihusisha timu za Geita Gold, JKT Kanembwa, JKT Oljoro na Polisi Tabora.
Viongozi watakaohojiwa na Kamati ya Nidhamu ni, Yusuf Kitumbo (Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tabora), Fateh Remtullah (Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tabaora), viongozi wa benchi la ufundi Polisi Tabora, Mrisho Selemani, Boniface Komba, Bernard Rabiamu.
Kamati pia itawahoji Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Geita, Salum Kurunge na mwenyekiti wa Klabu ya JKT Oljoro, Amos Mwita.
No comments