HUYU NDIYE ATAKAYECHEZA NAFASI YA N'GOLO KANTE BAADA YA KUUMIA LEICESTER CITY

Taarifa za kuumia kwa kiungo wa Leicester City Ngolo Kante ambaye ataikosa michezo miwili ya timu yake dhidi kuanzia mchezo wa leo dhidi ya West Bromwich Albion na mchezo unaofuata  katika ligi kuu nchini England zimepokelewa kwa maono tofauti na Wapenda Soka duniani wengi wakiamini kwamba sasa lile anguko la Leicester City ndilo  limefika.


Andy King 

Lakini hali ni tofauti kwa kocha mkuu wa timu hiyo Claudio Ranieri kwani ameshathibitisha kwamba Nafasi ya N'golo Kante itajazwa  na mchezaji Andy King ambaye hana wasiwasi nae na anaamini kwamba huu ni wakati wake mkongwe huyu kuonekana.
King - kushoto

Andy King ndiye mchezaji aliyedumu na Leicester City kwa kipindi kirefu zaidi tangu alipojiunga na klabu hiyo inayotumia uwanja wa King Power mwaka 2004.

Kante ambaye amekua ndiye mhimili wa mafanikio ya Leicester City msimu huu alitolewa katika mechi iliyopita dhidi ya Norwich ambapo Leicester City iliibuka na ushindi wa bao 1-0 akisumbuliwa na maumivu  ya  misuli ya paja.
N'golo Kante - kulia






Leicester City wanaoongoza ligi hiyo leo watakua nyumbani kuwakaribisha West Bromwich Albion katika mchezo ambao watu wengi wanataka kuona kama Leicester City bila N'golo Kante inawezekana na macho yote yatakuwa kwa ANDY KING

No comments

Powered by Blogger.