KOMBE LA FA : MAN CITY VS CHELSEA, MAN UNITED MTEREMKO

Michuano ya kombe la chama cha soka nchini England FA itaingia katika hatua ya 16 bora kwa Ratiba kamili kupangwa Jumapili hii baada ya kukamilika  michezo ya Raundi  ya nne.



Pambano ambalo lime vita hisia za mashabiki wa soka duniani ni pambano baina ya Manchester City dhidi ya Chelsea

Man City  wametinga hatua hii baada ya kuwaondoa Aston Villa huku Chelsea wakiitupa nje MK  Dons. Pambano hiki litakua kama fainali baada ya timu zote hizo kuwa na vikosi Imara.

Kwa Upande wa Manchester United wao wamepata mteremko  baada ya kupangiwa timu ya daraja la pili (league 1) ya Shrewsbury town timu pekee ya daraja la chini iliyobaki  katika michuano hiyo kutoka ligi za chini.

Mabingwa watetezi  Arsenal wao wamepangwa  kukutana na Hull City katika hatua hii mechi itakayopigwa katika uwanja wa Emirates jijini London.

HII NDIYE RATIBA KAMILI YA MECHI ZA RAUNDI YA 5 (16 BORA)


Chelsea vs Manchester City
Reading vs West Brom or Peterborough
Watford vs Leeds United
Shrewsbury Town vs Manchester United
Blackburn vs Liverpool/ West Ham
Tottenham vs Crystal Palace
Arsenal vs Hull
Bournemouth vs Everton

No comments

Powered by Blogger.