MAN UNITED YAIKANYAGA DERBY COUNTY MARA 3 KOMBE LA FA
Mechi za Hatua ya nne ya michuano ya kombe la FA nchini England zilianza jana kwa Manchester United kuibuka na ushindi wa bao 3-1 wakiifunga timu ya daraja la kwanza ya Derby County.
Wayne Rooney alitangulia kufunga dakika ya 16 ya mchezo akipokea pasi ya Anthony Martial na kufunga bao lake la 243 kwa klabu hiyo.
George Thorne aliisawazishia Derby kwa kufunga bao safi lililodumu mpaka mapumziko.
Kipindi cha pili Man United ilicharuka na kuongeza mashambulizi wakimtumia zaidi Anthony Martial na kufanikiwa kupata bao mbili zikifungwa na Daley Blind na Juan Mata
Kwa matokeo hayo Man United inatinga hatua ya Tano ya michuano hiyo yenye historia kubwa kwa soka la England
Wayne Rooney alitangulia kufunga dakika ya 16 ya mchezo akipokea pasi ya Anthony Martial na kufunga bao lake la 243 kwa klabu hiyo.
George Thorne aliisawazishia Derby kwa kufunga bao safi lililodumu mpaka mapumziko.
Kipindi cha pili Man United ilicharuka na kuongeza mashambulizi wakimtumia zaidi Anthony Martial na kufanikiwa kupata bao mbili zikifungwa na Daley Blind na Juan Mata
Kwa matokeo hayo Man United inatinga hatua ya Tano ya michuano hiyo yenye historia kubwa kwa soka la England
No comments