STARS YAENDELEA KUJIFUA UTURUKI
Timu ya Taifa ya
Tanzania (Taifa Stars) ipo nchini Uturuki, imeendelea na mazoezi jana asubuhi
katika viwanja viliyopo kwenye viunga vya hoteli ya Green Park – Kartepe.
Mara baada ya kuwasili
jumatatu jioni katika eneo la Kartepe, timu ilifanya mazoezi jioni kwa
takribani saa moja na nusu, kuanzia saa 1 jioni mpaka mida ya saa 3 kasoro
usiku, ambapo leo na kesho itafanya mazoezi asubuhi na jioni.
Kocha Mkuu wa Taifa
Stars, Charles Mkwasa amesema huduma na vifaa vilivyopo katika hoteli
waliyofikia (viwanja, gym) wanavyotumia kwa ajili ya mazoezi ni vizuri, hivyo
ratiba yake ya mazoezi inakwenda kama alivyopanga katika maandalizi ya wiki
moja ya kuajiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria.
Taifa Stars
inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa mazoezi na timu ya Taifa ya Libya
siku ya ijumaa, ambapo kocha Mkwasa atatumia nafasi hiyo kupima kikosi chake
baada ya kuwa wamefanya mazoezi kwa siku nne nchini Uturuki.
Kikosi cha wachezaji
21 chini ya kocha mkuu Charles Mkwasa, na msaidizi wake Hemed Morocco, kocha wa
makipa Peter Manyika na mshauri wa benchi la ufundi Abdallah Kibadeni
wanaendelea kuwanoa vijana vilivyo kwa ajili ya mchezo wa mwezi Septemba dhidi
ya Nigeria.
No comments