MAAJABU KOMBE LA FA - CHELSEA,MAN CITY,SOUTHAMPTON NA SPURS ZATUPWA NJE..

Patrick Blomfed akishangilia goli alilowafunga Man City
Maajabu ya kombe la FA pale England yameendelea kuonekana baada ya jana Manchester United United kutoka sare ya bila kufungana na timu ya daraja la pili ya Cambridge United leo michezo kadhaa imepigwa na kushuhudiwa vigogo wa ligi ya England wakitupwa nje.


Mechi hizo za Raundi ya nne zimemalizika muda mfupi uliopita na kushuhudiwa Vinara wa Ligi Kuu England Chelsea wakitupwa nje kwa kufungwa bao 4-2 nyumbani kwao Stamford Bridge na klabu ya daraja la Championship Bradford City.
Wachezaji wa Chelsea wakitoka uwanjani vichwa chini

Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Nchini England Manchester City wao walikubali kichapo cha bao 2-0 nyumbani Etihadi toka kwa Middlesbrough timu nyingine inayoshiriki Championship.

Southampton ambao msimu huu wameonekana wako vizuri na kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi walikubali kichapo cha bao 3-2 toka kwa Crystal Palace ambayo imeongezwa nguvu kufatia kumpata kocha mpya Allan Pardew pambano hilo lilipigwa nyumbani kwa Southamptob St. Marys stadium.
Chamakh,zaha,campbel na Sanogo wakishangilia

Klabu zingine za Ligi kuu ambavyo vimepata vichapo leo ni pamoja na Swansea City waliokubali kichapo cha bao 3-1 toka kwa Blackburn Rovers ambayo nayo inashiriki Ligi ya Championship.

MATOKEO YOTE YA KOMBE LA FA LEO


  • Blackburn Rovers 3-1 Swansea
  • Birmigham City 1-2 West Brom
  • Cardiff City 1-2 Reading
  • Chelsea 2-4 Bradford City
  • Derby County 2-0 Chesterfield 
  • Manchester City 0-2 Middlesbrough
  • Preston 1-1 Sheffield United
  • Southampton 2-3 Crystal Palace
  • Sunderland 0-0 Fulham
  • Tottenham Hotspurs 1-2 Leicester City

~ Edo Daniel Chibo

No comments

Powered by Blogger.