ARGENTINA YA MESSI HOI KWA URENO: YAPIGWA 1-0.


Pambano la kimataifa la kirafiki kati ya Argentina na Ureno limemalizika kwa Ureno kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Alikua kijana mdogo Raphael Guerreiro aliyepeleka kilio kwa Argentina akicheza mchezo wake wa pili akiwa na Ureno na kufanikiwa kufunga bao pekee dakika za lala salama goli ambalo limepelekea Ushindi kwa Ureno baada ya kusota zaidi ya miaka 40 wakitafuta ushindi dhidi ya Argentina.

Lionel Messi na Cristiano Ronaldo walicheza dakika 45 za mwanzo na hawakurudi kwa kipindi cha pili. Lakini wakali wengine kama Carlos Tevez,Angel Di Maria waliweza kuonekana kipindi cha pili katika pambano ambalo lilikua na ubabe mwingi na burudani ya kutosha. k

No comments

Powered by Blogger.