HIVI NDIVYO MAMA YAKE ADIN DZEKO ALIVYOMWOKOA MWANAE NA KIFO
Edin Dzeko.
Mkali wa mabao Raia wa Bosnia Hezgovina , mwenye miaka 28 anayekipiga katika klabu ya Manchester City ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi kuu England (EPL).
Ni kati ya wachezaji wachache wanaojua lugha nyingi kwani Dzeko anaongea vizuri lugha ya Kibosnia, Kiczech, Kijerumani na Kiingereza.
Historia ya mchezaji huyu katika soka imetawaliwa na mambo mengi ya kusikitisha kwani Amecheza sana mpira wa mtaani kama walivyo wachezaji wengi ila bahati mbaya kwake amekulia kwenye nchi iliyopigana vita ya wenyewe kwa wenyewe
enzi hizo ikiitwa Yugoslavia.
Sarajevo ndo mji aliokulia, mji uliokumbwa na machafuko ya kisiasa kwa mda mrefu kupelekea watu wengi kupoteza maisha yao.
Mama yake, Belma anasema Edin alikua mtundu sana, alikua akimkataza kwenda kucheza mpira viwanjani, kwa sababu mabomu yalikua yanapigwa hasa sehemu za halaiki. Lakini Edin alikua akipenya kwenye fensi, akisubiriwa na wenzake, na wanaenda viwanjani kusakata soka ambalo leo limemfanya awe milionea.
Siku moja, mama yake Edin, alimfungia mwanae huyo, ndani, akampa chakula na kumuwashia televisheni. Edin alilaani na kulia sana akisema mechi hiyo ilikua ni muhimu asingeweza kukosa. Hata chakula alizira kula siku hiyo kumuonyesha mama yake kama alikwazika.
Ni maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine yameitengeneza "career" ya Edin na kumweka hai mpaka leo.
Hiyo ndiyo siku ambayo ilihifadhi mambo mengi tunayoyaona hivi sasa kwa Edin Dzeko kwani ni siku ambayo kiwanja alichozoea kucheza Edin na wenzake, kilipigwa mabomu ya angani, na watoto wote waliokua uwanjani hapo wakifurahia soka walifariki baada ya kupigwa na mabomu hayo. Na moja kati ya waliokufa alikua ni binamu yake Edin Dzeko aliyejulikana kwa jina la Alexanda Dzeko.
Baada ya tukio hilo Mama yake alimpeleka kanisani, na wakasali sana, akiamini Mungu ana mipango na mwanae.
Baadae alipata bahati ya kwenda kusoma nje ya nchi na hapo ndipo alipotokea.
Leo hii Edin Dzeko ni mchezaji muhimu kwenye kikosi cha kifahari cha Manchester City kikosi ambacho amekiongoza kushinda makombe mawili ya Ligi kuu nchini England, ameshinda pia Kombe la ligi (Capital One), kombe la FA mara moja na Ngao ya jamii mara moja
Amewahi pia kutwaa ubingwa wa Ujerumani na club ya Wolfsburg msimu wa 2008/2009. Yeye akitwaa kiatu cha mfungaji bora, akifunga magoli 30.
HUYU NDO EDIN DZEKO
{ Fankinho WS}
Mkali wa mabao Raia wa Bosnia Hezgovina , mwenye miaka 28 anayekipiga katika klabu ya Manchester City ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi kuu England (EPL).
Ni kati ya wachezaji wachache wanaojua lugha nyingi kwani Dzeko anaongea vizuri lugha ya Kibosnia, Kiczech, Kijerumani na Kiingereza.
Historia ya mchezaji huyu katika soka imetawaliwa na mambo mengi ya kusikitisha kwani Amecheza sana mpira wa mtaani kama walivyo wachezaji wengi ila bahati mbaya kwake amekulia kwenye nchi iliyopigana vita ya wenyewe kwa wenyewe
enzi hizo ikiitwa Yugoslavia.
Sarajevo ndo mji aliokulia, mji uliokumbwa na machafuko ya kisiasa kwa mda mrefu kupelekea watu wengi kupoteza maisha yao.
Mama yake, Belma anasema Edin alikua mtundu sana, alikua akimkataza kwenda kucheza mpira viwanjani, kwa sababu mabomu yalikua yanapigwa hasa sehemu za halaiki. Lakini Edin alikua akipenya kwenye fensi, akisubiriwa na wenzake, na wanaenda viwanjani kusakata soka ambalo leo limemfanya awe milionea.
Siku moja, mama yake Edin, alimfungia mwanae huyo, ndani, akampa chakula na kumuwashia televisheni. Edin alilaani na kulia sana akisema mechi hiyo ilikua ni muhimu asingeweza kukosa. Hata chakula alizira kula siku hiyo kumuonyesha mama yake kama alikwazika.
Ni maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine yameitengeneza "career" ya Edin na kumweka hai mpaka leo.
Hiyo ndiyo siku ambayo ilihifadhi mambo mengi tunayoyaona hivi sasa kwa Edin Dzeko kwani ni siku ambayo kiwanja alichozoea kucheza Edin na wenzake, kilipigwa mabomu ya angani, na watoto wote waliokua uwanjani hapo wakifurahia soka walifariki baada ya kupigwa na mabomu hayo. Na moja kati ya waliokufa alikua ni binamu yake Edin Dzeko aliyejulikana kwa jina la Alexanda Dzeko.
![]() |
Dzeko wa nne toka kushoto waliochuchumaa |
Baada ya tukio hilo Mama yake alimpeleka kanisani, na wakasali sana, akiamini Mungu ana mipango na mwanae.
Baadae alipata bahati ya kwenda kusoma nje ya nchi na hapo ndipo alipotokea.
Leo hii Edin Dzeko ni mchezaji muhimu kwenye kikosi cha kifahari cha Manchester City kikosi ambacho amekiongoza kushinda makombe mawili ya Ligi kuu nchini England, ameshinda pia Kombe la ligi (Capital One), kombe la FA mara moja na Ngao ya jamii mara moja
Amewahi pia kutwaa ubingwa wa Ujerumani na club ya Wolfsburg msimu wa 2008/2009. Yeye akitwaa kiatu cha mfungaji bora, akifunga magoli 30.
HUYU NDO EDIN DZEKO
{ Fankinho WS}
No comments